Chama cha wachimba madini cha DRC kimeitaka serikali kufanya mazungumzo ya dharura ili kufafanua kanuni mpya za usafirishaji wa kobalt, baada ya mfumo wa quota kuibua utata wa kisheria na kuchelewesha mauzo ya nje. DRC, inayozalisha zaidi ya 70% ya kobalt duniani, imeweka kiwango cha usafirishaji na masharti mapya ya malipo ya mapema, lakini kampuni nyingi zimeshindwa kuyatimiza, jambo lililosimamisha usafirishaji. Wachimbaji wanatahadharisha kuwa hatua zisizo wazi zinaweza kudhoofisha uaminifu wa kimataifa wa sekta hiyo na kuathiri mnyororo wa usambazaji wa betri duniani.
CHANZO: TRT Afrika














