Rais Donald Trump amezindua visa maalum ya ‘Trump Gold Card’, ambayo itagharimu angalau dola milioni 1 na kutoa njia ya moja kwa moja ya kupata uraia wa Marekani kwa wanaostahiki. Mpango huo unaeleza kuwa waombaji lazima waonyeshe manufaa makubwa watakayoipelekea Marekani. Hatua hii inakuja wakati ambapo serikali ya Trump imeongeza msako dhidi ya wahamiaji haramu na kuongezea ada za visa za kazi. Biashara zitakazofadhili wafanyakazi zitatozwa dola milioni 2, huku toleo jipya la ‘platinamu’ la dola milioni 5 likiahidi punguzo maalum la kodi.
CHANZO: BBC NEWS














