Shambulio la ndege zisizo na rubani limeua raia saba na kujeruhi wengine 12 katika hospitali ya jeshi mjini Dilling, kusini mwa Sudan, kulingana na wahudumu wa afya. Tukio hilo linajiri huku mapigano kati ya jeshi la Sudan na RSF yakiendelea, na Umoja wa Mataifa ukionya juu ya hali mbaya ya kibinadamu na njaa inayowaathiri wakazi wa eneo hilo.
CHANZO: TRT Afrika














