Kampuni ya teknolojia ya ulinzi nchini Nigeria, Terra Industries, imezindua mifumo mipya ya ulinzi inayojitegemea ikiwemo ndege zisizo na rubani za kukamata mashambulizi, magari ya kugundua mabomu, na programu za ujasusi wa vita.
Maonesho hayo, yaliyofanyika Jumatatu mbele ya maafisa wa ngazi ya juu wa jeshi na serikali, yanaashiria mabadiliko ya kampuni hiyo kutoka kutoa huduma za usalama wa miundombinu hadi kutengeneza teknolojia za moja kwa moja kwa matumizi ya Jeshi la Nigeria.
Mifumo iliyoonyeshwa inajumuisha magari yasiyo na dereva yenye uwezo wa kugundua mabomu ya kutegwa pamoja na ndege zisizo na rubani zinazoweza kuzuia mashambulizi ya anga kwa kugongana moja kwa moja na shabaha.
CHANZO: TRT Afrika














