Serikali ya Australia imetangaza mkakati mpya wa kitaifa wa kupambana na semi za chuki na misimamo mikali baada ya shambulio la risasi lililotokea Bondi, Sydney, ambapo watu 15 waliuawa wakati wa sherehe za Hanukkah. Waziri Mkuu Anthony Albanese amesema sheria hizo zitalenga wanaochochea chuki, mgawanyiko na vurugu, huku Waziri wa Mambo ya Ndani akipewa mamlaka ya kufuta au kukataa visa kwa wahusika wa aina hiyo. Hatua hizo pia zinajumuisha kuanzishwa kwa kosa jipya la shirikisho la semi za chuki iliyoimarishwa, adhabu kali kwa vitisho na unyanyasaji mtandaoni, pamoja na kuundwa kwa kikosi kazi cha elimu ili kukabiliana na chuki dhidi ya Wayahudi. Ingawa hatua hizo zimeibua wasiwasi kuhusu uhuru wa kujieleza, serikali imesisitiza kuwa lengo lake ni kulinda usalama, mshikamano wa taifa na haki ya kila raia kuishi bila hofu.
CHANZO: BBC NEWS









