Zaidi ya watu 200, wakiwemo wanawake na watoto, wameuawa katika mashambulizi mapya ya kikabila yaliyotekelezwa katika maeneo ya Kaskazini na Magharibi mwa Darfur, kulingana na taarifa ya Madaktari wa Sudan.
Taarifa hiyo imesema kuwa raia walilengwa moja kwa moja katika miji ya Ambro, Abu Qamra na Sirba baada ya mashambulizi yaliyodaiwa kufanywa na vikosi vya Rapid Support Forces (RSF). Waliokimbia mapigano walieleza kuwa mauaji yalifanyika kwa misingi ya kikabila.
Madaktari hao wameeleza mashambulizi hayo kuwa ukiukaji mkubwa wa sheria za kimataifa za kibinadamu, huku RSF ikiwa haijatoa tamko rasmi.
Mashambulizi hayo yanakuja wakati mapigano yakiendelea kuongezeka Darfur, huku pande zinazopigana zikilaumiana kwa kuwalenga raia na kuchoma vijiji, hali inayozidisha mgogoro ambao umeua maelfu na kuwafanya mamilioni kukimbia makazi yao tangu ulipoanza mwaka 2023.
CHANZO: TRT Afrika














