Serikali ya Tanzania imefafanua kuhusu kukamatwa kwa meli iliyokuwa na bendera ya Tanzania nchini El Salvador baada ya kudaiwa kubeba tani 6.6 za dawa za kulevya aina ya cocaine.
Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema meli hiyo ilisajiliwa Zanzibar lakini inamilikiwa na raia wa kigeni na hakukuwa na Mtanzania yeyote aliyekuwemo ndani ya chombo hicho wakati wa tukio.
Aliongeza kuwa Serikali ya Zanzibar tayari ilifuta usajili wa meli hiyo kutokana na kukosekana kwa ushirikiano kutoka kwa wamiliki wake, pamoja na kuchukua hatua nyingine za kisheria.
CHANZO: TRT Afrika














