Uturuki Siasa

Erdogan: Kipaumbele ni kuilinda Uturuki isivutwe vitani

Recep Tayyip Erdoğan amesema kipaumbele cha Uturuki ni kuepuka kuingia katika vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati.

Newstimehub

Newstimehub

14 Mechi, 2026

485

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan amesema serikali yake inachukua tahadhari kubwa ili kuhakikisha nchi hiyo haivutwi katika vita vinavyoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati.

Alisema Ankara inaendelea kuwa makini dhidi ya mipango, mitego na uchochezi wowote unaoweza kuingiza Uturuki katika mzozo huo.

Kauli hiyo imekuja wakati mvutano katika kanda ukiongezeka kufuatia mashambulizi dhidi ya Iran na mashambulizi ya kulipiza kisasi kutoka Tehran.

CHANZO: TRT Afrika