Mgombea mmoja tu ndiye atashindana na Rais wa Djibouti Ismail Omar Guelleh katika uchaguzi wa rais wa nchi hiyo mwezi ujao, kulingana na notisi rasmi.
Djibouti ina takriban watu milioni moja katika eneo la kimkakati karibu na Bahari Nyekundu na Ghuba ya Aden, na ni nyumbani kwa kambi muhimu za kijeshi za Marekani , Uchina, Ufaransa na mataifa mengine.
Guelleh, 78, ametawala nchi hiyo tangu 1999, atawania muhula wa sita Aprili 10 baada ya wabunge kwa kauli moja kufanyia marekebisho katiba mwezi Novemba ili kuondoa ukomo wa umri wa miaka 75.
Chanzo: TRT Afrika














