Mkuu wa shirikisho la soka la Iran amesema kuwa hadi sasa hakuna visa zilizotolewa kwa timu ya taifa kushiriki katika Kombe la Dunia la 2026 nchini Marekani, vyombo vya habari vya serikali viliripoti.
“Kesho au keshokutwa tutakuwa na mkutano muhimu na FIFA. Lazima watupe dhamana kwa sababu suala la visa bado halijatatuliwa,” shirika la habari la serikali la IRNA limemnukuu mkuu wa shirikisho hilo, Mehdi Taj.
“Hatujapokea taarifa yoyote kutoka upande wa pili kuhusu nani amepewa visa. Bado hakuna visa zilizotolewa,” aliongeza.
Timu ya Iran itafanya mazoezi ya kujitayarisha na michuano ya Kombe la Dunia 2026 nchini Uturuki.
















