Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameagiza Kituo cha Tafiti za Kiuchumi, Kijamii na Uchambuzi wa Sera (ZRCP) kuandaa mikutano na mijadala na wadau ili kuwaelimisha umuhimu wa kutumia matokeo ya tafiti katika utekelezaji wa majukumu yao.
Akizungumza Machi 24, 2026, alipokutana na Mkurugenzi Mkuu wa ZRCP, Juma Reli, Rais Mwinyi pia amesisitiza maboresho ya mifumo ya malipo ya kidijitali katika sekta ya umma, huku akishauri upya wa sera, sheria na kanuni.
CHANZO: TRT Afrika














