Katika kipindi ambacho mvutano kati ya Iran, Marekani na Israel unaongezeka, kumekuwepo na ukimya wa kushangaza kutoka kundi la Al-Qaeda.
Wachambuzi wanasema hali hiyo inaweza kuonyesha kuwa kundi hilo halina uwezo mkubwa wa kuathiri mwelekeo wa vita au linaepuka kujiingiza moja kwa moja.
Kihistoria, Al-Qaeda imekuwa ikipinga Marekani, lakini pia ina tofauti za kiitikadi na Iran, ambayo ni ya madhehebu ya Shia, tofauti na msimamo wa Sunni wa Al-Qaeda.
Hivyo, ukimya huo unaweza kuwa ni mkakati wa kuepuka kuchukua upande wazi katika mgogoro mgumu wa kisiasa na kidini.
Baadhi ya wataalamu wanaamini kuwa kundi hilo linajaribu kujipanga upya au kusubiri fursa ya kutumia hali hiyo kwa propaganda.
Chanzo:BBC Swahili
















