Shirika la misaada la Médecins Sans Frontières (MSF) limeripoti kuongezeka kwa kasi kwa visa vya ugonjwa hatari wa meningitis katika mashariki mwa Chad, hali iliyosababisha vifo vya takriban asilimia 12 ya watoto walioambukizwa.
Kwa mujibu wa MSF, watoto 212 walilazwa kati ya Machi na Aprili, ambapo 25 walifariki dunia, kiwango kilichoelezwa kuwa cha kutisha.
Hali hiyo imezidishwa na uwepo wa wakimbizi wengi kutoka Sudan, ambao wamekimbia vita vinavyoendelea tangu mwaka 2023.
Mashariki mwa Chad, hasa katika maeneo ya mpakani, imekuwa kitovu cha dharura ya afya kutokana na msongamano mkubwa wa watu.
















