Meli ya mizigo imeripotiwa kutekwa karibu na pwani ya Somalia baada ya watu wasiojulikana kuichukua na kuielekeza ndani ya maji ya eneo hilo, kwa mujibu wa Shirika la Uingereza la Ufuatiliaji wa Biashara za Baharini (UKMTO).
Tukio hilo limeripotiwa kutokea takribani maili 6 za baharini kaskazini mashariki mwa Garacad, Somalia. UKMTO ilisema watu hao walichukua udhibiti wa meli hiyo na kuibadilishia mwelekeo kuelekea maji ya ndani ya Somalia.
Mamlaka za baharini zimezitaka meli zote zinazopita eneo hilo kuwa makini na kutoa taarifa kuhusu shughuli zozote zinazotia shaka wakati uchunguzi ukiendelea.
CHANZO: TRT Afrika














