Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) imelaani vikali mashambulizi ya kigaidi yaliyotokea Aprili 25, 2026 katika maeneo mbalimbali ya Mali, ikiyataja kuwa ni matendo ya kinyama yanayoonesha ukatili wa wahusika wake.
Katika taarifa yake, ECOWAS imezitaka nchi wanachama, vikosi vya usalama, mifumo ya kikanda pamoja na wananchi kuungana katika juhudi za pamoja kukabiliana na tishio la ugaidi linaloendelea kuhatarisha usalama wa Afrika Magharibi.
Jumuiya hiyo pia imetoa salamu za rambirambi kwa familia za waathiriwa na kueleza mshikamano wake kamili na serikali pamoja na wananchi wa Mali.
CHANZO: TRT Afrika














