Shirikisho la Soka Zimbabwe (ZIFA) limetangaza kuwa kocha wa timu ya taifa ya nchi hiyo, Marian Marinica, amejiuzulu kutoka wadhifa wake kwa sababu binafsi ambazo hazijawekwa wazi.
Marinica mwenye umri wa miaka 61 aliteuliwa mwezi Novemba mwaka jana kwa mkataba wa mwaka mmoja kuinoa timu ya taifa ya Zimbabwe.
Kocha huyo wa Romania alikuwa na uzoefu wa awali wa kuongoza timu za taifa za Malawi na Liberia kabla ya kupewa jukumu la kuinoa Zimbabwe.
Kuondoka kwake kunakuja bila matarajio ya wengi huku akiwa bado ndani ya kipindi chake cha mkataba.














