Kundi la benki la Kenya, Equity Group, limetangaza kuwa linatafuta fursa za kununua taasisi za kifedha nchini Angola, Zambia na Msumbiji kama sehemu ya mkakati wake wa kupanua uwepo wake barani Afrika.
Afisa Mkuu Mtendaji wa kampuni hiyo, James Mwangi, amesema masoko hayo yanaonyesha ukuaji mkubwa kutokana na maendeleo ya miundombinu, biashara ya kikanda na utajiri wa madini kama shaba na cobalt.
Mwangi alieleza kuwa mkakati wa Equity si kuingia tu katika nchi mpya, bali kufuata wateja wake na njia kuu za biashara katika ukanda huo.
Hatua hiyo inakuja baada ya mafanikio ya benki hiyo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambako sasa ni benki ya pili kwa ukubwa baada ya ununuzi wa benki mbili mwaka 2015 na 2020.
CHANZO: TRT Afrika
















