Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed, amesema nchi yake haina “nia ya kupanua mipaka” wala kutishia majirani zake, akisisitiza kuwa upatikanaji wa bandari na matumizi ya maji ya Nile ni masuala ya msingi kwa taifa. Katika ujumbe alioutoa kwa Kiarabu kuelekea Ramadan, Abiy alieleza kuwa juhudi za Ethiopia kupata ufikiaji wa bahari ni “hitaji la kimsingi la kimaisha” linalotokana na ongezeko la idadi ya watu na mahitaji ya maendeleo.
Aliongeza kuwa hatua hiyo ni mwaliko wa ushirikiano na si tishio kwa uhuru wa majirani. Kuhusu Nile, Abiy alisema kuwa rasilimali hiyo ni “zawadi ya pamoja” inayopaswa kuimarisha ushirikiano badala ya kuleta migogoro.
CHANZO: AA














