Ulimwengu Afrika

Benki ya Dunia na Qatar kushirikiana kusambaza umeme kwa watu milioni 300 Afrika

Makubaliano pia yanajumuisha kutengeneza ajira na kusaidia nchi zilizoathiriwa na migogoro.

Newstimehub

Newstimehub

26 Januari, 2026

362

Benki ya Dunia (WBG) na Mfuko wa Maendeleo wa Qatar (QFFD) wamesaini makubaliano ya ushirikiano wa kimkakati yatakayosaidia kupanua upatikanaji wa umeme kwa watu milioni 300 Kusini mwa Jangwa la Sahara. Makubaliano hayo, yaliyotiwa saini mjini Doha, pia yanajumuisha kutengeneza ajira, kusaidia nchi zilizoathiriwa na migogoro ya silaha, na kuimarisha uchumi wa maeneo yanayoibuka.

Mpango huu unajumuisha utekelezaji wa M-300, unaolenga kuongeza huduma za umeme barani Afrika, na AgriConnect, jukwaa la Benki ya Dunia litakaloboresha maisha ya wakulima wadogo milioni 250 duniani.

Fahad Hamad Al-Sulaiti, Mkurugenzi Mkuu wa QFFD, alisema hatua hiyo inaendana na Dira ya Taifa ya Qatar 2030, huku Rais wa Benki ya Dunia Ajay Banga akisisitiza kuwa ushirikiano huo utakuza ajira na fursa za kiuchumi kwa uthabiti wa muda mrefu.

CHANZO: TRT Afrika