Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, amesema kuwa kipengele cha ulinzi wa pamoja cha Umoja wa Ulaya si maneno matupu bali kina nguvu ya vitendo.
Akizungumza wakati wa ziara nchini Ugiriki, Macron alieleza kuwa nchi wanachama wa EU tayari wameonyesha mshikamano kwa kusaidiana kijeshi pale kunapokuwa na tishio.
Alitoa mfano wa msaada wa haraka uliotolewa kwa Cyprus baada ya tukio la shambulio, akisema hilo linaonyesha uwezo wa EU kujilinda yenyewe.
Kauli hiyo inakuja wakati kukiwa na wasiwasi kuhusu utegemezi wa Ulaya kwa NATO na Marekani katika masuala ya usalama.
Viongozi wa EU sasa wanapanga kuweka mfumo rasmi wa jinsi kipengele hicho kitakavyotumika kwa vitendo wakati wa dharura.
Chanzo:The Guardian
















