Afrika

Mahakama Kuu Kenya yaendelea kuzuia mpango wa kujenga kituo cha Ebola

Kumekuwa na hali ya wasiwasi kufuatia hatua ya serikali ya kutaka kuweka kituo cha karantini kwa jili ya raia wa Marekan huku ikiibua maswali kuhusu afya ya umma, uwazi katika mchakato huo, pamoja na masuala ya kikatiba na mamlaka ya taifa.

Newstimehub

Newstimehub

2 Juni, 2026

67dd6fca16904dc721459fef10edbe40cb6ca545aae092a832bb698efb9b6a40

Mahakama Kuu nchini Kenya imetoa amri ya muda ya kuzuia Serikali kuanzisha, kuendesha, kuwezesha au kuruhusu kuanzishwa kwa kituo chochote cha karantini, au cha matibabu ya Ebola nchini Kenya chini ya makubaliano yanayopangwa kati ya Kenya na Marekani au serikali nyingine yoyote ya kigeni.

Mahakama pia imepiga marufuku kuruhusiwa kuingia kwa watu walioathiriwa au walioambukizwa Ebola chini ya mpango huo hadi pale ombi na kesi iliyowasilishwa mahakamani litakaposikilizwa na kuamuliwa.

Hatua hiyo imechukuliwa kufuatia maswali yaliyoibuliwa kuhusu afya ya umma, uwazi katika mchakato huo, pamoja na masuala ya kikatiba na mamlaka ya taifa.

Kwa upande wake, akizungumzia suala hilo, Rais William Ruto alitetea mpango huo akisema kuwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha utayari wa Kenya katika kukabiliana na magonjwa ya kuambukiza, na si tishio kwa usalama wa wananchi.