Serikali ya United States imetangaza kuwa inapanga kupunguza takriban wanajeshi 5,000 walioko nchini Germany.
Hatua hiyo inakuja wakati kukiwa na mvutano wa kisiasa kati ya kiongozi wa Marekani Donald Trump na kiongozi wa Ujerumani Friedrich Merz kuhusu masuala ya ushirikiano wa kijeshi na matumizi ya fedha katika ulinzi,Kwa mujibu wa maafısa wa Marekani, hatua hiyo ni sehemu ya tathmini ya upya ya uwepo wa kijeshi barani Ulaya, huku ikilenga kupunguza gharama na kupanga upya vikosi.
Hata hivyo, wachambuzi wanasema kuwa uamuzi huo unaweza kuathiri ushirikiano wa kijeshi kati ya nchi hizo mbili pamoja na usalama wa eneo la Ulaya kwa ujumla,
Serikali ya Ujerumani imeeleza kuwa itaendelea kushirikiana na Marekani licha ya hatua hiyo, huku ikisisitiza umuhimu wa mshikamano ndani ya muungano wa kijeshi wa NATO.
Chanzo:BBC News














