Marekani imetangaza vikwazo dhidi ya rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Joseph Kabila, kwa madai ya kutoa msaada kwa kundi la waasi la AFC/M23 linalopigana mashariki mwa nchi hiyo.
Kupitia Idara ya Hazina ya Marekani, Washington imesema Kabila anatuhumiwa kutoa msaada wa kifedha kwa waasi hao pamoja na kuwahimiza wanajeshi wa Congo kujitenga na kujiunga nao.
Hatua hizo zinajumuisha kufungiwa kwa mali zake zote zilizopo nchini Marekani na kupigwa marufuku kwa raia au taasisi za Marekani kufanya biashara naye.
CHANZO: TRT Afrika
















