Mgogoro unaoendelea katika Mashariki ya Kati umeathiri vibaya sekta ya mauzo ya nyama ya Kenya, huku usafirishaji ukishuka hadi chini ya asilimia 5 ya kiwango cha kawaida wakati wa msimu wa Ramadhani.
Sababu kuu ni kuongezeka kwa gharama za usafiri wa anga na kupungua kwa safari za ndege, hali iliyowalazimu wauzaji kutumia njia ghali zaidi za kusafirisha bidhaa. Gharama za kusafirisha kilo moja zimeongezeka zaidi ya mara mbili.
Hali hiyo imeathiri mnyororo mzima wa uzalishaji kutoka wafugaji hadi machinjio na baadhi ya nyama inalazimika kuuzwa ndani ya nchi kwa bei ya chini.
Chanzo: TRT Afrika














