Jeshi la Egypt limefanya mazoezi ya kijeshi ya kutumia risasi halisi katika eneo lililo karibu na mpaka wake na Israel.
Kwa mujibu wa taarifa za jeshi, mazoezi hayo ni sehemu ya mpango wa kawaida wa kuimarisha uwezo wa vikosi vya ulinzi katika kukabiliana na vitisho mbalimbali vya kiusalama.
Mazoezi hayo yalihusisha matumizi ya silaha nzito, magari ya kijeshi na uratibu wa vikosi vya ardhini, yakilenga kuongeza utayari wa wanajeshi katika hali za dharura.
Hatua hiyo imekuja wakati kukiwa na mvutano katika baadhi ya maeneo ya Mashariki ya Kati, jambo ambalo limezua tahadhari kwa nchi jirani.
Hata hivyo, mamlaka za Misri zimesisitiza kuwa mazoezi hayo hayalengi kuchochea mgogoro wowote bali ni sehemu ya maandalizi ya kawaida ya kijeshi.
Chanzo:Africanews














