Serikali ya Misri imetangaza kugundua hifadhi mpya ya gesi asilia katika eneo la Delta ya Nile, hatua inayotarajiwa kuongeza uzalishaji wa nishati nchini humo.
Wizara ya Petroli na Rasilimali Madini ya Misri imesema ugunduzi huo ulifanyika baada ya uchimbaji wa mafanikio wa kisima cha utafiti cha Nidoco N-2 katika eneo linaloendeshwa na kampuni ya Italia Eni kwa ushirikiano na BP ya Uingereza.
Kwa mujibu wa wizara hiyo, kisima hicho kinatarajiwa kuzalisha takriban futi za ujazo milioni 50 za gesi kwa siku.
CHANZO: TRT Afrika














