Mkuu wa Pentagon, Pete Hegseth, anatarajiwa kutoa ushuhuda wake wa kwanza mbele ya Bunge la Congress siku ya Jumatano kuhusu vita vinavyoendelea kati ya Marekani na Iran, wakati juhudi za kidiplomasia za kumaliza mzozo huo zikiwa hazijazaa matunda.
Hegseth atahojiwa mbele ya Kamati ya Huduma za Kijeshi ya Bunge la Wawakilishi, katika kikao kitakachojadili pia bajeti ya kijeshi ya mwaka 2027 inayopendekeza matumizi ya dola trilioni 1.5 katika sekta ya ulinzi.
Wanademokrat wamekuwa wakikosoa vita hivyo, wakisema vilianzishwa bila idhini ya Congress na vinaweza kuwa mzigo mkubwa wa kifedha kwa Marekani.
Katika ushuhuda wake, Hegseth anatarajiwa kueleza sababu za kuongezwa kwa matumizi ya kijeshi, ikiwemo mahitaji ya drones zaidi, mifumo ya ulinzi wa makombora na meli za kivita.
















