Afrika

Mnigeria Hilda Baci aweka rekodi Guinness kwa kupika kilogramu 8,780 za wali

Upishi wa mlo huo ulifanyika ndani ya chombo chenye ujazo wa lita 22,000, ukitumia nishati ya gesi ya zaidi ya kilo 1,200 ndani ya saa tisa.

Newstimehub

Newstimehub

16 Septemba, 2025

5fe240564ee4c9763cf0f0facce7d0d039cf0e8c7906bd5dfec959e401994e8c

Mpishi maarufu wa Nigeria Hilda Effiong Bassey, ameingia kwenye vitabu vya rekodi za dunia za Guinness baada ya kufanikiwa kupika kiwango kikubwa cha wali aina ya Jollof, ambao ni mlo maaurufu nchini Nigeria.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa siku ya Jumatatu, mpishi huyo, ambaye anatambulika kwa jina maarufu la Hilda Baci, aliweka rekodi hiyo akiwa katika eneo la Victoria Island jijini Lagos, baada ya kufanikiwa kupika wali wenye kilo 8,780.

38b0f9cffd0b7c619413a0c886e864b04e3976a8dff439a7644d868afc3136c1 1