Mpishi maarufu wa Nigeria Hilda Effiong Bassey, ameingia kwenye vitabu vya rekodi za dunia za Guinness baada ya kufanikiwa kupika kiwango kikubwa cha wali aina ya Jollof, ambao ni mlo maaurufu nchini Nigeria.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa siku ya Jumatatu, mpishi huyo, ambaye anatambulika kwa jina maarufu la Hilda Baci, aliweka rekodi hiyo akiwa katika eneo la Victoria Island jijini Lagos, baada ya kufanikiwa kupika wali wenye kilo 8,780.















