Afrika Ajenda

Rwanda yashirikiana na Ghana kutuma wahandisi Jamaica baada ya kimbunga Melissa

Kikosi cha RDF kimepelekwa Jamaica kusaidia ukarabati wa miundombinu iliyoharibiwa na majanga.

Newstimehub

Newstimehub

14 Januari, 2026

273

Rwanda imepeleka kikosi cha wahandisi wa kijeshi nchini Jamaica kusaidia katika ukarabati wa miundombinu iliyoharibiwa na Kimbunga Melissa mwishoni mwa Oktoba 2025. Hatua hiyo imefanyika kwa mujibu wa makubaliano ya ushirikiano kati ya Rwanda na Jamaica, kulingana na taarifa ya Jeshi la Ulinzi la Rwanda (RDF).

Ingawa idadi ya wahandisi haikufichuliwa, kikosi hicho kilipokea maelekezo kutoka kwa Brigedia Jenerali Faustin Tinka kabla ya safari yao kutoka Kigali. Tinka aliwahimiza kutumia utaalamu na weledi wao ili kufanikisha jukumu walilopewa.

Jamaica ndiyo iliyoathirika zaidi na kimbunga hicho, ambacho kilisababisha vifo na hasara kubwa inayokadiriwa kufikia dola bilioni 8.8 za Marekani. Mnamo Disemba, Ghana tayari ilituma wahandisi 54 wa kijeshi kusaidia katika juhudi za kujenga upya miundombinu muhimu.

CHANZO: TRT Afrika