Serikali ya Tanzania imeanzisha mikakati mipya ya kudhibiti upatikanaji na usambazaji wa mafuta kwa kuunda timu maalum inayojumuisha vyombo vya ulinzi na usalama. Lengo ni kuhakikisha mafuta yanafika kwa wakati na hayakosekani sokoni.
Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema changamoto kubwa si bei ya mafuta bali ni upatikanaji wa mafuta ghafi duniani. Ameeleza kuwa wakati mwingine mafuta yanakuwepo maghalani lakini hayasambazwi kwa haraka kwa watumiaji.
CHANZO: TRT Afrika














