Tanzania imetuma mwaliko rasmi kwa wabunge wa Marekani kutembelea nchi hiyo mwakani, kufuatia mazungumzo kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na mjumbe wa Bunge la Marekani Ronny L. Jackson. Mwaliko huo unakuja wakati Marekani ikitathmini upya uhusiano wake na Tanzania, huku pande zote zikijadili kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na kimataifa.
CHANZO: TRT Afrika














