Rais wa Nigeria Bola Tinubu amekubali kimsingi kuyafutia mashirika ya ndege ya ndani madeni yanayodaiwa na mawakala wa usafiri wa anga baada ya mazungumzo kati ya wadau.
Hatua hiyo inakuja baada ya mashirika ya ndege kutishia kusitisha huduma zao kuanzia Aprili 20 kutokana na kupanda kwa gharama za mafuta ya ndege.
Kwa mujibu wa Waziri wa Usafiri wa Anga Festus Keyamo, rais ameagiza kuwasilishwa kwa ombi rasmi ili kuamua kiwango cha punguzo la madeni hayo.
Serikali pia imetangaza kuunda kamati maalum itakayopitia kodi, ushuru na ada mbalimbali katika tiketi za ndege ili kupunguza mzigo kwa mashirika na abiria.
CHANZO: TRT Afrika














