Usalama Afrika

UN Yaweka Vikwazo kwa Kiongozi wa RSF na Mamluki Watatu wa Colombia Sudan

Baraza la Usalama lashutumu uhusika wa usajili wa wanajeshi wa zamani wa Colombia katika vita vya Sudan.

Newstimehub

Newstimehub

29 Aprili, 2026

734

Umoja wa Mataifa kupitia Baraza la Usalama umeweka vikwazo dhidi ya Algoney Hamdan Daglo Musa, mdogo wa kiongozi wa kikosi cha Rapid Support Forces (RSF) nchini Sudan, pamoja na raia watatu wa Colombia wanaodaiwa kuhusika katika kusajili wapiganaji wa zamani kwenda kupigana nchini Sudan.

Kwa mujibu wa taarifa ya ujumbe wa Uingereza katika UN, vikwazo hivyo vimewekwa kufuatia mapendekezo ya Marekani, Uingereza na Ufaransa kutokana na ushahidi wa ushiriki wao katika vita vinavyoendelea Sudan.

Algoney Hamdan Daglo Musa anadaiwa kuratibu ununuzi wa silaha na vifaa vya kijeshi kwa ajili ya RSF, kundi linaloongozwa na kaka yake Mohamed Hamdan Dagalo.

CHANZO: TRT Afrika