Zaidi ya watu 30 wanahofiwa kupoteza maisha nchini Uganda baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama katika Ziwa Nguse usiku wa Jumanne.
Kwa mujibu wa taarifa za awali, watu hao walikuwa wakirejea kutoka msitu wa Bugoma walikokwenda kuvuna mkaa kabla ya ajali hiyo kutokea katika kijiji cha Kyaleni, Manispaa ya Pachwa.
Msemaji wa Polisi wa eneo la Albertine, Julius Hakiiza, amesema hadi sasa mwili mmoja umeopolewa huku juhudi za uokoaji na utafutaji zikiendelea.
Uchunguzi wa awali umebaini kuwa boti hiyo huenda ilizidiwa uwezo baada ya kubeba watu wengi kuliko kiwango kinachoruhusiwa.
CHANZO: TRT Afrika














