Teknolojia

xAI yaweka vizuizi kwa Grok kufuatia lawama za picha za faragha

Tumetekeleza hatua za kiteknolojia kuzuia Grok kuhariri picha za watu halisi katika mavazi ya kufichua mwili.

Newstimehub

Newstimehub

15 Januari, 2026

282

Kampuni ya Elon Musk, xAI, imetangaza kuwa chatbot yake ya AI, Grok, haitaruhusiwa kuhariri picha za watu halisi ili kuwaonesha katika mavazi ya kufichua mwili katika maeneo ambako jambo hilo ni kinyume cha sheria. Hatua hii imekuja baada ya malalamiko makubwa ya kimataifa kuhusu matumizi mabaya ya kipengele cha “spicy mode” kilichowezesha utengenezaji wa picha za faragha zisizo na ridhaa.

Serikali kadhaa, ikiwemo Malaysia na Indonesia, tayari zimechukua hatua za kisheria na kufunga Grok, huku Umoja wa Ulaya, Uingereza, India na Ufaransa wakitoa onyo kali. Brazil na California pia zimeanzisha uchunguzi rasmi, zikieleza kuwa Grok imerahisisha utengenezaji wa picha za “deepfake” zinazotumika kuwatishia na kuwanyanyasa wanawake na wasichana mtandaoni.

Kwa mujibu wa xAI, sasa huduma za kuunda au kuhariri picha zimewekewa masharti kwa watumiaji wanaolipia pekee, ili kuhakikisha wanaokiuka sheria au sera wanaweza kuwajibishwa. Mamlaka ya California imesema ripoti za hivi karibuni kuhusu kusambazwa kwa picha za faragha zisizo na ridhaa ni “za kutisha,” na imeonya kuwa hakuna uvumilivu kwa maudhui ya aina hiyo.

CHANZO: TRT Afrika