Maporomoko ya ardhi yaliyosababishwa na mvua kubwa hivi majuzi katika eneo la uchimbaji madini ya coltan mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yaliua watu 10 na wengine kadhaa kupotea, vyombo vya habari vya ndani viliripoti Jumamosi.
Maporomoko hayo ya ardhi yalitokea mwendo wa saa nne asubuhi Jumamosi katika eneo la uchimbaji madini la Rubaya katika eneo la Masisi Kaskazini mwa Kivu, kufuatia mvua kubwa iliyonyesha, kulingana na Radio Okapi.
Miili dazeni ilitolewa saa sita mchana, ikiwa ni pamoja na watoto sita, ripoti ilisema, ikinukuu mashahidi.
Chanzo: TRT Afrika














