Shirika la ujasusi la Somalia limesema zaidi ya wanamgambo 22 wa Al-Shabab wameuawa katika operesheni mbili zilizofanyika katika maeneo ya kati ya nchi hiyo.
Kwa mujibu wa NISA, operesheni hizo zililenga viongozi wa kundi hilo pamoja na maeneo wanayojificha.
Mamlaka zimesema mashambulizi hayo ni sehemu ya juhudi za kuondoa kabisa kundi hilo katika maeneo linapojificha.
CHANZO: TRT Afrika














