Afrika

Rais wa DRC anataka kufufua Shirika la Ndege la Congo Airways

Baada ya kusimamisha ndege zake zote kutokana na wasiwasi wa usalama, Congo Airways imetegemea ndege za kukodishwa ambazo zina gharama kubwa.

Newstimehub

Newstimehub

22 Mechi, 2026

37f330392a2d3affcbef764a85b3ed72902bfe7f6b0d3e4c150546553fd33674

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Felix Tshisekedi ameagiza mamlaka husika kuja na mpango mkakati mpya utakaosaidia kufufua Shirika la Ndege la nchi hiyo, Congo Airways.

Shirika hilo linalomilikiwa na serikali na kubeba bendera ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), limekuwa likikabiliwa na changamoto ya fedha, migogoro ya matengenezo, na kusimamishwa mara kwa mara kwa safari za ndege zake.

Baada ya kusimamisha ndege zake zote kutokana na wasiwasi wa usalama, Congo Airways imekuwa ikitegemea ndege za kukodisha ambazo ni gharama kubwa.

Rais Tshisekedi alitoa maagizo ya kufufuliwa kwa shirika hilo la ndege wakati wa mkutano wa 83 wa Baraza la Mawaziri, kulingana na ripoti iliyotangazwa kwenye televisheni ya taifa.

“Rais alimuagiza Naibu Waziri Mkuu, Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Waziri wa Fedha na Waziri wa Mashirika ya Nchi, chini ya usimamizi wa Waziri Mkuu, akisaidiwa na wizara nyingine husika na mashirika ya umma, kuandaa mpango ulioboreshwa, wa kweli na wenye muundo madhubuti wa kuokoa Congo Airways,” ripoti ilisema.

“Ripoti hiyo inapaswa kujumuisha mbinu za wazi za udhibiti wa ndani, uzingatiaji wa kanuni, ukaguzi wa kina, usimamizi wa rasilimali watu, na ripoti ya kawaida ya kitaasisi kwa Serikali na mwenye hisa,” ripoti hiyo ilisema.

Ndege za shirika hilo ambazo ni pamoja na ndege nne, mbili zikiwa Airbus A320 zilizuiliwa mapema mwaka 2024 kutokana na injini iliyoisha muda wake, gharama kubwa za matengenezo ya zaidi ya Dola za Marekani milioni 28, na masuala ya usalama.

Operesheni zilisitishwa mara nyingi, mnamo Septemba 2023 na tena mnamo Julai 2024 na kulazimisha kutegemea ukodishaji wa muda mfupi wa ndege kwa gharama kubwa.

Mpango wa mabadiliko uliowasilishwa mwishoni mwa Januari 2025 unajumuisha upatikanaji wa ndege tatu za Airbus kwa kukodisha au kununua ndani ya miaka mitano, pamoja na kupanga upya utawala.

Mpango huo unategemea msaada wa kifedha kutoka kwa mamlaka ya umma ikiwa ni pamoja na serikali ya DRC.

Timu mpya ya usimamizi iliteuliwa mnamo Januari 2025 lakini mchakato huo ulikwama.

Katika mkutano wake wa hivi punde na wajumbe wa baraza la mawaziri Rais Tshisekedi pia aliagiza kwamba ripoti inayoelekeza mkakati wa kurudisha fahari hiyo ya nchi pia kuongoza jinsi ya kurekebisha usimamizi wa kampuni, kwa nia ya kurejesha nidhamu na uwajibikaji wa viongozi wake.