Aliyekuwa Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete, ameteuliwa na Tume ya Umoja wa Afrika kuwa Mwakilishi Mkuu wa Pembe ya Afrika na Bahari ya Shamu. Katika nafasi hiyo, atashughulikia masuala ya kisiasa, amani na usalama katika ukanda huo.
Atafanya kazi kwa ushirikiano na taasisi za kikanda na kimataifa kama IGAD, EAC, Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu ili kuimarisha utulivu wa eneo hilo muhimu kwa biashara ya kimataifa.
CHANZO: TRT Afrika














