Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema kuwa hakuna mazungumzo yoyote yanayoendelea kati ya Iran na Marekani, akisisitiza kuwa mawasiliano kupitia wapatanishi hakuashirii kuwepo kwa mazungumzo rasmi.
Araghchi amesema viongozi wa ngazi ya juu wa Iran wanaendelea kupitia mapendekezo yaliyowasilishwa, lakini akabainisha wazi kuwa nchi hiyo haina nia ya kuanzisha mazungumzo na Marekani kwa sasa.
Aidha, ameeleza kuwa Iran haitafuti vita, bali inalenga kufikia mwisho wa kudumu wa mzozo uliopo pamoja na kupata fidia kwa uharibifu uliosababishwa.
Chanzo: TRT Afrika














