Kesi ya uhalifu inayomkabili Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu imeahirishwa kufuatia sababu za kiusalama, kwa mujibu wa uamuzi wa mahakama ya wilaya ya Yerusalemu.
Majaji waliamua kuendelea kusikiliza ushahidi kutoka kwa shahidi mwingine badala ya kumuita Netanyahu kizimbani, hatua iliyochelewesha ushahidi wake uliokuwa unatarajiwa.
Uamuzi huo ulifuatia ombi kutoka kwa upande wa utetezi uliotaja masuala ya usalama kama sababu kuu, licha ya upinzani kutoka kwa waendesha mashitaka waliotaka kesi iendelee kama ilivyopangwa.
CHANZO: TRT Afrika














