Jeshi la Nigeria limeanzisha rasmi mahakama ya kijeshi (court martial) kuwashughulikia zaidi ya wanajeshi 30 wanaotuhumiwa kuhusika katika mpango wa mapinduzi uliodaiwa kufanyika mwaka 2025.
Kwa mujibu wa mamlaka za ulinzi, jumla ya wanajeshi 36 wanatarajiwa kushtakiwa kwa makosa ya uasi (mutiny) na jaribio la kuipindua serikali iliyopo madarakani.
Majaji wa mahakama hiyo waliapishwa rasmi, huku kesi zikitarajiwa kuendeshwa kwa siri (closed doors) kutokana na unyeti wa suala hilo la usalama wa taifa.
Hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za serikali ya Nigeria kukabiliana na kile ilichokiita jaribio hatari ambalo lingeweza kumaliza utawala wa kidemokrasia uliodumu kwa zaidi ya miaka 20.
Wakati huo huo, baadhi ya washukiwa raia tayari wamefikishwa katika mahakama za kiraia na kushtakiwa kwa uhaini na ugaidi, huku wakikana mashtaka hayo.
Chanzo:Africanews
















