Serikali ya Mauritius imeelezea wasiwasi mkubwa kufuatia shambulizi la kombora lililolenga Kisiwa cha Chagos usiku wa Machi 19 kuelekea Machi 20.
Kupitia Wizara ya Mambo ya Nje, mamlaka zimesema tukio hilo ni ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa na linaweka hatarini amani na utulivu wa eneo la Bahari ya Hindi.
Mauritius imezitaka pande zinazohusika kusitisha mapigano mara moja na kurejea kwenye mazungumzo ya kidiplomasia ili kuepusha kuongezeka kwa mgogoro.
CHANZO: TRT Afrika














