Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amefanya mazungumzo kwa simu na Rais wa Marekani Donald Trump kufuatia jaribio la shambulio lililotokea wakati wa hafla ya White House Correspondents’ Dinner mjini Washington.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki, Erdogan alimweleza Trump mshikamano wake na kuilaani vikali tukio hilo.
Kiongozi huyo wa Uturuki alisema shambulio hilo ni kitendo cha kinyama kinacholenga demokrasia na uhuru wa vyombo vya habari.
Aidha, Erdogan alimtakia afisa wa usalama aliyejeruhiwa kupona haraka.














