Ulimwengu

Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz azomewa baada ya kuzinadi sera za serikali

Moja wa washiriki wa kongamano hilo, alimjia juu kiongozi huyo kufuatia matamshi yake ya hivi karibuni ya kuwataka Wajerumani waongezewe muda wa kufanya kazi.

Newstimehub

Newstimehub

15 Mei, 2026

1778848388349 kqq3v af715de609e608bbea7d03d552830e0e67d62a4c2e5bbb4cdbe16deecec73274

Kansela Friedrich Merz wa Ujerumani alijikuta kwenye wakati mgumu siku ya Ijumaa, baada ya kuzinadi sera za serikali ya Ujerumani.

Kansela huyo alizomewa wakati wa kongamano la Wakatoliki katika eneo la Wurzburg, baada ya baadhi ya washiriki kuonesha kutopendezwa na sera za kiuchumi na mazingira za serikali ya Ujerumani.

Moja wa washiriki wa kongamano hilo, alimjia juu kiongozi huyo kufuatia matamshi yake ya hivi karibuni ya kuwataka Wajerumani waongezewe muda wa kufanya kazi.

Mshiriki huyo, pia aliikosoa serikali ya Ujerumani ya kubadilisha mfumo mzima wa mifuko ya hifadhi ya jamii, akilalamikia kupanda kwa gharama za maisha chini humo.

“Hakuna mtu yeyote ndani ya chama change aliyewahi kusema kuwa Wajerumani ni watu wavivu,” alisema Merz.