Baadhi ya nchi za Asia zimeanza kurejesha mfumo wa kufanya kazi kutoka nyumbani ili kupunguza matumizi ya mafuta kufuatia kupanda kwa bei duniani. Mataifa kama Indonesia, Vietnam na Thailand yameanza kuchukua hatua za kupunguza safari zisizo za lazima na matumizi ya nishati.
Serikali zinasema kuwa kupunguza usafiri kunaweza kupunguza matumizi ya mafuta kwa kiwango kikubwa, huku zikilinda uchumi wao ambao umeanza kuathirika kutokana na mgogoro unaoendelea Mashariki ya Kati.
CHANZO: TRT Afrika














