Ajenda Usalama

Niger Yasitisha Shughuli za Zaidi ya NGO 2,900

Serikali ya kijeshi yasema hatua hiyo inalenga uwazi na kulinda vipaumbele vya taifa.

Newstimehub

Newstimehub

23 Aprili, 2026

659

Serikali ya Niger imesitisha shughuli za zaidi ya mashirika yasiyo ya kiserikali 2,900 kati ya 4,700 yaliyokuwa yamesajiliwa nchini humo.

Hatua hiyo ilitangazwa na waziri wa mambo ya ndani chini ya uongozi wa Abdourahmane Tiani, ambaye amekuwa madarakani tangu mapinduzi ya Julai 2023.

Kwa mujibu wa serikali, baadhi ya NGO zimekosa uwazi katika shughuli zao na zingine zimeshutumiwa kuunga mkono makundi yenye misimamo mikali.

Mohamed Toumba alisema idadi ya mashirika sasa imepungua hadi 1,800, akisisitiza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya “kusafisha” sekta hiyo.

Serikali pia imetaka mashirika yaliyosalia kuendana na vipaumbele vya maendeleo ya kitaifa.

CHANZO: TRT Afrika