Rais wa Marekani Donald Trump amekubali kusitisha mashambulizi dhidi ya Iran kwa kipindi cha wiki mbili, hatua iliyokuja muda mfupi kabla ya tarehe ya mwisho aliyoweka kwa mashambulizi makubwa.
Makubaliano hayo yamepatikana baada ya juhudi za upatanishi, huku Iran ikikubali kufungua Mlango wa Hormuz kwa usafirishaji salama wa mafuta.
Trump amesema hatua hiyo inalenga kutoa nafasi ya kukamilisha mazungumzo ya amani, akieleza kuwa tayari pande hizo zimekaribia kufikia makubaliano ya muda mrefu.
Hata hivyo, wataalamu wanaonya kuwa bado kuna tofauti kubwa kati ya pande hizo, na mustakabali wa makubaliano ya kudumu haujulikani.
Chanzo: Africanews














