Sehemu ya Ikulu iliyoko Nairobi imebainika kuvamia ardhi ya hifadhi ya Mto Kirichwa, baada ya ukaguzi uliofanywa na mamlaka husika.
Mamlaka ya Rasilimali za Maji imethibitisha kuwa ukuta wa Ikulu upo ndani ya umbali wa mita 15 kutoka kiwango cha juu cha maji ya mto huo, jambo linalokiuka sheria za mazingira.
Hatua hiyo imeibua mjadala mkubwa kuhusu ulinzi wa mazingira hata katika maeneo ya juu ya serikali.
CHANZO: TRT Afrika














