Serikali ya Kenya imepandisha bei ya mafuta ya rejareja baada ya kupanda kwa bei ya mafuta ghafi duniani kufuatia mzozo wa Mashariki ya Kati.
Kwa mujibu wa Energy and Petroleum Regulatory Authority (EPRA), lita moja ya petroli imeongezeka hadi shilingi 206.97 huku dizeli ikifikia shilingi 206.84.
Mamlaka hiyo ilieleza kuwa gharama za uagizaji zimepanda kwa kiasi kikubwa, jambo lililolazimu kupandisha bei hizo.
CHANZO: TRT Afrika














